Jumatatu, 28 Desemba 2015

Ukoloni ni Nini??

Ramani ya ukoloni duniani mwishoni mwa Vita Kuu ya Pili ya Dunia mwaka 1945.
Ukoloni ni mfumo wa taifa moja kuvuka mipaka yake na kutawala maeneo ya mbali yanayokaliwa na watu wengine kwa nyanja za kiuchumikiutamadunina kijamii. Maeneo haya yanaweza kuitwa koloni au eneo lindwa.
Ukoloni unaitwa hasa kipindi tangu karne ya 15 ambako Ureno na Hispaniazilianza kuenea Afrika na Amerika ya Kusini na kudumu hadi baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Lakini kulikuwa na vipindi vya ukoloni pia zamani katika historia kama vile ukoloni wa Roma ya Kale, ukoloni wa Waarabu na vingine. Ukoloni kwa maana hii inaweza kuwa tofauti na kuundwa kwa koloni katika vipindi mbalimbali vya historia ambako maeneo bila wakazi au penye wakazi wachache sana yaliingiliwa na watu kutoka sehemu nyingine.

Nchi za Afrika ziliwekwa chini ya ukoloni wa nchi za Ulaya mara baada yaMkutano wa Berlin ulioitishwa nachansella wa Ujerumani Bismarckmwaka 1884-1885.
Nchi zilizojenga ukoloni huu wa Afrika zilikuwa UingerezaUfaransaUreno,UjerumaniUhispaniaItalia na Ubelgiji.
Ukoloni mamboleo ni aina ya nchi au kundi la nchi fulani kutawala nchi nyingine kinyemela kwa kuweka vikwazo na masharti yatakayowafanya watawaliwa waendelee kuwa na uchumi tegemezi ili wawatajirishe zaidi hao wanaowatawala kinyemela

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni