Ijumaa, 22 Januari 2016

Picha ya karne ya 19 inayoonyesha wakazi wa Australia wakipinga kuwasili kwa Kapteni James Cook mwaka 1770
Uvumbuzi wa utamaduni unaamanisha uvumbuzi wowote mpya na unaopatikana kuwa wa manufaa kwa kikundi cha watu na unaelezewa katika tabia zao lakini haupo kama kitu kinachoonekana. Watu wako katika ulimwengu unaoharakisha mabadiliko ya utamaduni kiwakati,wakisukumwa na kupanuka kwa biashara kimataifa,vyombo vya habari,na kuongezeka kwa idadi ya watu miongoni mwa mambo mengine.
Tamaduni zinaathiriwa na nguvu zinazoleta mabadiliko na zile zinazopinga mabadiliko. Nguvu hizi zina uhusiano na miundo ya kijamii na matukio halisi na zinajihusisha katika kuendeleza mawazo na matendo ya kitamaduni ndani ya miundo ya sasa ambayo nayo inabadilika[186]. (Tazamaumuundo.)
Mizozo ya kijamii na maendeleo ya kiteknolojia yanaweza kusababisha mabadiliko katika jamii kwa kubadili mikikimikiki ya kijamii kwa kukuza ruwaza mpya za utamaduni kwa kuwezesha tukio zalishi. Hii mihamisho ya kijamii huweza kuandamana na mihamisho ya kiitkadi na aina nyingine za mabadiliko ya kitamaduni. Kwa mfano muungano wa kifeministi wa Kimarekani ulihusisha matendo mapya yaliyosababisha uhamisho katika mahusiano ya kijinsia,kubadilisha jinsia na miundo ya kiuchumi. Hali ya kimazingira inaweza kuchangia. Mabadiliko huhusisha kufuata nguli wa kienyeji katika filamu. Kwa mfano,misitu ya kitropika ilirejea tena mwishoni mwa enzi ya theluji.mimea iliyofaa kwa kufugwa ilikuwepo,ikasababisha kuvumbuliwa kwa kilimo,ambacho kilisababisha uvumbuzi wa kitamaduni na mihamisho ya mikikimikiki ya kijamii[187].
Picha kamili ya mwanamke wa Turkman,akisimama kwenye zulia katika mlango wa yurt,akiwa amevalia nguo za kitamaduni pamoja na virembesho
Tamaduni huathirika kutoka nje kupitia kwa mwingiliano baina ya jamii,ambazo pia zinaweza kutoa—au kuzuia---mihamisho ya kijamii na mabadiliko katika matendo ya kitamaduni. Vita au ushindani juu ya rasilimali unaweza kuathiri maendeleo ya kiteknolojia na mikikimikiki ya kijamii. Kuongezea,mawazo ya kitamaduni yanaweza kuhama kutoka jamii moja hadi nyingine kupitia kwa kuenea na kwa mabadiliko ya uigaji wa utamaduni Fulani. Katika kuenea hali ya kitu(siyo lazima maana yake) hutoka utamaduni mmoja hadi mwingine. Kwa mfano,hamburgers ambazo ni za kawaida Marekani,zilionekana kuwa ngeni zilipoanzishwa Uchina. "Kuenea kunakoacha athari” (kubadilishana mawazo) hurejelea elementi za utamaduni mmoja kusababisha kuwepo kwa uvumbuzi au kusambazwa.kwa mwingine. "Ukopaji wa moja kwa moja” kwa upande mwingine hurejelea kuenea kwa kiteknolojia au kuenea kunakoonekana kutoka utamaduni mmoja hadi mwingine. Nadharia ya kuenea kwa uvumbuzi huwasilisha ruwaza ya utafiti ya kwa nini na lini watu na tamaduni huasilisha mawazo mapya,matendo na bidhaa.
Kuiga utamaduni fulani kuna maana tofauti lakini katika muktadha huu hurejelea kubadilishwa kwa tabia Fulani za utamaduni na utamaduni mwingine.Haya yamefanyika kwa makabila fulani ya Amerika na kwa makundi asilia ya watu kote ulimwenguni enzi za ukoloni. Michakato ya karibu kwa kiwango cha binadamu inahusisha usilimisho (binadamu kuasilisha utamaduni fulani) na kuwa na tamaduni nyingi.

                     Utamaduni

Michoro mwambani huko Gobustan,Azerbaijan10000 KK ikionyesha utamaduni uliostawi.
Jumba la Kiajemi Hasht-Behesht.
Utamaduni ni jinsi binadamuanavyokabili maisha katika mazingirayake.
Neno la Kilatini lenye maana ya utamaduni ni Cultura ambalo lina usuliwake katika neno colere, linalomaanisha "kulima, kustawisha".[1]
Neno hili linafafanuliwa namna nyingi. Kwa mfano, mnamo mwaka 1952,Alfred Kroeber na Clyde Kluckhohnwalikusanya orodha ya vijelezi 164 vya neno hilo katika kazi yao: Culture:a Critical Review of Concepts and Definitions.[2]
Hata hivyo, neno "utamaduni" linatumika kimsingi katika njia tatu zifuatazo:
  • Maonjo ya hali ya juu katika sanaa, vilevile hujulikana kama utamaduni wa juu
  • Mkusanyo wa maarifa ya binadamu,itikadi na tabia ambao hutegemea sana uwezo wa kuwasilisha mawazo na mafunzo ya kijamii kwa njia ya ishara
  • Jumla ya mitazamo, kaida, malengona maadili yanayotambulisha asasi,shirika au kikundi fulani
Dhana hii ilipoibuka kwanza katikakarne ya 18 na 19 barani Ulaya, ilimaanisha mchakato wa kulima au kuboresha kilimo au kilimo cha mboga. Katika karne ya 19 dhana hii ilimaanisha kuboreshwa kwa mja kupitia elimu na hali kadhalika ilimaanisha kutekelezwa kwa maazimio ya kitaifa au maadili.
Katikati ya karne ya 19, wanasayansiwengine walitumia dhana ya utamaduni kurejelea uwezo wa kiubia wa binadamu.
Katika karne ya 20, "utamaduni" ulijitokeza kama dhana ya msingi katikasomo la Anthropolojia. "Utamaduni" ulihusisha mambo yote ya binadamu ambayo hayakufungamana namaumbile.
Dhana ya utamaduni katikaAnthropolojia ya Kimarekani ilikuwa na maana mbili: (1) Uwezo wa binadamu wa kuainisha na kuwasilisha tajiriba za kibinadamu kiishara na kutenda mambo kiubunifu; na (2) Namna mbalimbali ambazo watu wanaoishi katika sehemu mbalimbali ulimwenguni huainisha na kuwasilisha tajiriba zao za maisha na kutenda mambo kiubunifu. Kufuatia vita vya pili vya dunia, dhana hii ilipata umaarufu ingawa kwa fafanuzi tofautitofauti katika taaluma kama vilesosholojia, mafunzo ya utamaduni,saikolojia ya mipangilio na mafunzo yausimamizi.

Jumatatu, 4 Januari 2016

KINJEKITILE NGWALE NA HISTORIA YENYE UTATA!

Kulikuwa na mateso na kulimishwa kwa nguvu.
Leo katika kupekua kwangu mtandaoni, nimekutana na historia mbili tofauti zinazomzungumzia Kinjekitile. Kilichonivutia hadi kuamua kuwashirkikisha wasomaji wa kibaraza hiki ili tutafakari kwa pamoja ni kutokana na kupingana kwa historia hizo.

Wakati historia moja ikihoji kuwa Kinjekitile alikuwa shujaa au mshirikina? ambayo iliandikwa na mwandishi Aloyce Menda katika gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Septemba 21,2006, nyingine ilikuwa ikidai kuwa historia yake imepotoshwa, ambayo nayo iliandikwa na mwandishi Evaristy Masuha katika gazeti hilo hilo la Tanzania Daima la Alhamisi, Agosti 21, 2008.

Kwa historia hizo mbili kunaonekana kuwa na walakini na ni vyema historia hii ikawekwa sawa kwa manufaa ya vizazi vijavyo, la sivyo tutajikuta tukiwa tumepoteza kumbukumbu hii muhimu kwa vizazi vyetu.

Naomba tuwekane sawa katika swala hili, Je ni yupi yuko sahihi kati ya waandishi hawa wawili?

***************************************

Alhamisi, 31 Desemba 2015


Kwa nini Mlima Kilimanjaro uko Tanzania na si Kenya?

Mlima Kilimanjaro
MPAKA wa Tanzania na Kenya ni wa ajabu na ni wa kushangaza pia. Tofauti na mipaka mingine ya nchi yetu upande wa Mashariki, Kusini na Magharibi, Mpaka huo wa Kaskazini umechorwa kwa mstari ulionyooka kana kwamba ulichorwa kwa msaada wa rula kuanzia Bahari ya Hindi, kuelekea Kaskazini hadi Ziwa Victoria.
Kwa jinsi ulivyoanza, mstari huo ulipaswa kwenda moja kwa moja Kaskazini Magharibi, na kuutupa nje Kaskazini Mlima Kilimanjaro uwe ndani ya Kenya, badala ya kuwa Tanzania ilivyo sasa. Lakini, pengine kwa sababu maalumu, mchoraji aliupaisha juu Kaskazini zaidi makusudi ulipokaribia Mlima huo, kisha ukapinda tena kuelekea Kaskazini Magharibi kwa unyoofu ule ule, kuhakikisha kwamba Mlima wote unakuwa ndani ya Tanzania badala ya Kenya; na kuendelea hadi Ziwa Victoria kwa kunyooka vivyo hivyo.
Kwa nini, nani kitu gani hasa kilimfanya mchoraji wa Mpaka huo kupindisha mstari huo kufanya Mlima Kilimanjaro uwe nchini Tanzania, badala ya kuwa nchini Kenya?
Mnyukano wa Wajerumani na Waingereza
Kuna dhana inayovuma kwamba, Malkia wa Uingereza, Victoria; alimpa zawadi mjukuu wake, mtawala (Emperor) wa Ujerumani, Wilhelm Mlima huo mwaka 1886, kwa sababu mjukuu huyo alipenda vitu vikubwa.  Dhana hii si sahihi kwa sababu mwaka huo, Wilhelm hakuwa mtawala wa Ujerumani, bali Babu yake. Lakini jibu sahihi linatokana na Mataifa ya Ulaya kugombea Afrika (Scramble for Africa), mnyukano uliokamilishwa na Mkutano wa Berlin kwa mataifa hayo kukaa meza moja kuchora mipaka (partition) kuigawana Afrika.
Mnyukano huo ulishika kasi ya kutisha katikati ya miaka ya 1880, Uingereza ikiongoza na kufuatiwa na Ufaransa; huku Ujerumani nayo ikijikakamua kutoachwa nyuma katika kuwania makoloni.
Desemba 4, 1884, Sultani Mangungu wa Usagara (Msovelo) alisainishwa Mkataba wa “Urafiki” na Jasusi la Kijerumani, Karl Peters, bila kujua kwamba alikuwa anauza nchi yake kwa Wajerumani na kuitwa “Deutch –Ostafrika”, yaani “Afrika Mashariki ya Wadachi/Wajerumani” na kuimilikisha Kampuni ya Kijerumani iliyojulikana kama “German East African Company” (GEAC).
Februari 1885, Karl Peters aliomba ulinzi wa Kampuni yake kwa Kiongozi wa Ujerumani (Emperor), Bismarck, na kupewa barua ya kukubaliwa (Imperial Letter of Protection) kupata ulinzi wa maeneo (nchi) yote yaliyochukuliwa na GEAC upande wa Bara Magharibi mwa Dar es Salaam, na maeneo ya Uzigua, Ukaguru na Usambara ambako machifu 10 wa maeneo hayo walisaini Mikataba “kumuuzia” nchi zao bila kujua.
Ilichotaka GEAC ni kupata njia huru na Bandari kwenye Bahari ya Hindi, na hivyo kuzua mgongano na Sultani wa Zanzibar aliyeshikilia Pwani yote, kutoka Somalia upande wa Kaskazini hadi Rasi Delgado (Msumbiji) upande wa Kusini; na pia Bara yote iliyokuwa njia ya misafara ya Watumwa hadi Maziwa Makuu.
Na pale Sultani Sayyid Barghash alipoonesha jeuri ya kutokubali matakwa ya Wajerumani, Manowari ya kivita ya Kijerumani ilitia nanga Bandari ya Zanzibar na kuelekeza mitutu ya mizinga kwenye Kasri lake, naye akasalimu amri hima.  Wakati huo Zanzibar ilikuwa chini ya usimamizi na ulinzi wa Uingereza (British Protectorate) kwa Mkataba maalumu.
Kuona hivyo, Februari 26, 1886, Waziri Mkuu wa Uingereza wa wakati huo, Lord Salisbury, aliingilia kati akiamini kwamba, haki za Zanzibar juu ya eneo lote la Pwani zilikuwa wazi, ingawa hakuwa na uhakika juu ya ukomo wake Kaskazini (Somalia?), lakini alifikiri umbali wa maili 60 ulimtosha Sultani. Alijua kuwa, himaya ya Sultani ilijumuisha pia Wilaya za Kilimanjaro na Uchagani; alisema:  “Eneo lote la Wilaya ya Kilimanjaro kamwe haliwezi kuwa chini ya ulinzi wa bendera nyingine (mbali ya Sultani au Uingereza) bila kuathiri maslahi ya Uingereza”.
Wababe wote walikuwa na mikataba
Ni kwamba, Waingereza, Wajerumani na Sultani mwenyewe, wote walikuwa na mikataba waliyoingia na Machifu wa Kichaga kutambua himaya za wababe hao, kama tu alivyofanya Chifu Mangungu.  Mmoja wa Mikataba ya Machifu hao 25 na Sultani, uliotiwa sahihi Mei 30, 1885, ulisomeka hivi:
“Sisi Masultani (machifu) wa Uchagani na Kilimanjaro, tunaapa mbele ya Jenerali Mathews na Askari wake na Wafuasi, kwamba, tunatambua kuwa (sisi) ni watawaliwa wa Mtukufu Sultani wa Zanzibar, na hivyo tunapeperusha bendera yake juu ya minara nchini mwetu kuthibitisha utii wetu kwake, na kuwa,tunamtambua kama mtawala/mfalme wetu”.
Mkataba huo wa pamoja ulitiwa sahihi (dolegumba) na Machifu Mandara wa Moshi, Kitungeti wa Kirua; Marealle wa Muranju (Marangu), Mitanuvi wa Mamba, Fumba wa Kilema, pamoja na Machifu wa Machame, Rombo, Taveta na wengineo.
Mandara alitia sahihi Mkataba mwingine kama huo na Mjerumani wa GEAC, Dakta Karl Juhlke, Juni 11, 1885, kumpa mamlaka yote na haki ya kuchukua na kutumia ardhi, kutoza kodi na ushuru, pamoja na kuanzisha utawala wake na Mahakama; kuvuna Mlima Kilimanjaro, Mito, Maziwa na Misitu yote.
Kubadilishana na haki hizo, Mandara alihakikishiwa ulinzi, yeye na mali zake, pamoja na elimu kwa watoto wake. Akitoa shukrani kwa Dakta Juhlke na GEAC, Mandara alisema: “Nawapenda sana Wajerumani kuliko mataifa mengine yote; zaidi kuliko Waingereza hasa, nani kwako pekee (wewe Juhlke) nitatoa nchi yangu”.
Hatimaye, baada ya kubaini kwamba alikuwa njia panda, Mandara alilalama akisema:  “Sultani wa Zanzibar anataka nchi yangu; Wajerumani, vivyo hivyo nao wanataka nchi yangu; ninyi (Waingereza) mnataka nchi yangu pia! Aitakaye nchi yangu atakiona cha mtema kuni”. Hakutaja aina ya “cha mtema kuni” hicho.
Tume ya maridhiano yaundwa
Kutokana na kindumbwendumbwe hicho, Uingereza, Ufaransa na Ujerumani ziliunda Tume ya Maridhiano kubainisha mipaka kwa kuzingatia maeneo ya ushawishi wa nchi hizo kuepuka ugomvi, lakini Sultani hakushirikishwa.
Mijadala ndani ya Tume ilikuwa mikali, kila mshiriki akivutia upande wake.  Mwakilishi wa Ujerumani alitaka kutumia Bandari ya Dar es Salaam iliyokuwa chini ya himaya ya Sultani, bila kutozwa kodi.
Pili, alitaka Sultani apunguziwe eneo la himaya upande wa Pwani ili abakie na urefu wa maili kumi tu; pia kwamba, madai ya Sultani huyo juu ya eneo la Kilimanjaro yasitambuliwe.
Tatu, Ujerumani ilitaka kampuni zote za Uingereza zilizokuwa eneo la Kilimanjaro ziondoke na zikubali kulipwa fidia ili Mjerumani ashike eneo lote hilo.
Kwa GEAC, Kilimanjaro lilikuwa jambo la kufa na kupona, na ilikuwa tayari kwa lolote kutoiachia; kama ambavyo tu Zanzibar ilivyokuwa muhimu kisiasa na kiuchumi kwa “Emperor”  Bismarck wa Ujerumani kiasi kwamba, nchi hiyo ilikuwa na Ubalozi mdogo Visiwani humo tangu mwaka 1884 kuonesha umuhimu huo.
Uingereza na Ufaransa zilionesha kuunga mkono madai ya Sultani dhidi ya matakwa ya Ujerumani. Kwa kupewa ujasiri na msimamo wa nchi hizo, wakati mazungumzo yakiendelea, Sultani alituma kikosi chenye Askari 200, kikiongozwa na Jemedari wa Kiingereza, Jenerali Mathews, kwenda eneo la Kilimanjaro kusimika bendera nyekundu ya himaya yake. Wakati wakirejea, walipambana na Kikosi cha Wajerumani karibu na Taveta, kilichofika huko kwa madhumuni hayo hayo; mapigano yakazuka, lakini yakakoma sawia kwa maelekezo ya Tume ya Maridhiano iliyokuwa ikiendelea na kikao.
Wakati huo huo, Mwakilishi wa Uingereza, Sir Percy Anderson, alikuja na wazo la kati katika kutatua ugomvi wa Ujerumani na Uingereza kuhusu eneo la Kilimanjaro, la kuligawa sehemu mbili kuwapa Wajerumani nusu ya upande wa Kusini, na nusu ya Kaskazini wapewe Waingereza.
Pendekezo hilo lilipingwa vikali na Wajerumani kwa madai kwamba isingekuwa rahisi kuligawa hivyo eneo hilo lenye mlima na vilima, hivyo wakasisitiza wapewe eneo lote peke yao. Sir Percy alitupa hoja yake kutafuta suluhu mbadala.
Mombasa yatibua mambo
Ikazuka hoja kuhusu nani adhibiti Mombasa (bandari) ambayo ilikuwa chini ya himaya ya Sultani, lakini yenye kuwaniwa vikali na Uingereza na Ujerumani pia.  Wajerumani walitaka wawe na Bandari Pwani ya eneo hilo na (iwe) njia fupi kuufikia Mlima Kilimanjaro kwa urahisi, na kwamba, Mombasa ulikidhi madhumuni haya kwavile ulikuwa katikati ya maeneo ambayo Ujerumani ilikuwa ikiwania upande wa Kaskazini na Kusini.
Waingereza hawakuwa tayari kupoteza Mombasa, kufa na kupona; kama ambavyo tu Wajerumani hawakuwa tayari kupoteza Kilimanjaro. Jemadari wa Kiingereza, Luteni Kanali Kitchner, tayari alikuwa ameshinikiza kukamatwa kwa Mombasa ili kiwe Kituo cha Manowari zakivita za Uingereza na ghala kuu la silaha katika bahari ya Hindi.
Nao wafanyabiashara na Wamissionari wa Kiingereza,walioweka vituo na Makao Mombasa, hawakutaka Serikali yao kuachia bandari hiyo pamoja na njia za biashara “kuangukia kwenye udhibiti wa Taifa shindani” kwani, kwa maoni ya Sir Percy, Uingereza ingekosabarabara ya uhakika hadi Ziwa Victoria “unakoanzia Mto Nile,na hivyo kuwa vigumu kuifikia Sudani ya Chini”. Kufikia hapo, mazungumzo yaligota na hali ya kutoaminiana kutawala.
Mpaka mpya:  Taveta hadi Victoria
Ili kukidhi matarajio yake, Sir Percy aliwasilisha pendekezo la pili, la Mpaka unaoanzia Kusini mwa Mombasa kuelekea Taveta, kisha unapanda juu sehemu ya Kaskazini mwa Kilimanjaro (kuuingiza ndani mlima huo), na kuambaa hadi Mashariki mwa kingo za Ziwa Victoria, kama unavyoonekana leo.
Kwa pendekezo hili la pili, Ujerumani iliamua kuachia Mombasa na kukubali kutia sahihi Mkataba wa makubaliano kwa kuridhika kwamba maeneo Kusini ya mpaka huo yaliyobakia mikononi mwake, yalikidhi kiu yake ya makoloni kufanya ijishughulishe kwa muda mrefu uliofuata.
Mkataba huo, uliofikiwa Novemba 1, 1886, ulielezea mpaka huo ifuatavyo:  “Mstari wa Mpaka unaanzia kwenye mdomo wa Mto Wanga au Umbe,unakwenda moja kwa moja hadi Ziwa Jipe; unapita upande wa Mashariki mwa Ziwa na kupinda tena upande wa Kaskazini kabla ya kuvuka mto Rumi; kisha unachana katikati ya nchi ya Taveita (Taveta) na Uchagga; unaambaa chini ya kitako cha Mlima Kilimanjaro kwenda juu kuelekea Kaskazini; kisha unanyooka tena moja kwa moja na kutua upande wa Mashariki wa kingo za Ziwa Victoria Nyanza”.
Huo ndio ufafanuzi kwa maneno ya kidiplomasia, wa Mpaka kati ya Tanganyika (wakati huo ikiitwa Deutch – Ostafrika) na Kenya uliopo hadi leo. Chini ya makubaliano hayo, Ujerumani, kupitia Kampuni ya GEAC, ilijipatia Mlima Kilimanjaro na kupoteza Mombasa; na Waingereza kujipatia Mombasa na kupoteza Mlima Kilimanjaro.
Januari 1, 1891, maeneo yote ya GEAC yaliingizwa kwenye himaya ya Serikali ya Ujerumani kuruhusu uvamizi na uingiliaji kijeshi wa maeneo hayo,yakiwa tayari milki halali ya nchi hiyo.
Kutoka Deutch – Ostafrika hadi Tanganyika
Sultani wa Zanzibar kwa upande wake, alibakiziwa kipande cha urefu wa maili 10 tu za Pwani, ambacho miaka miwili baadaye, mwaka 1888, alikikodisha kwa Wajerumani kisha akapokonywa kwa nguvu mwaka huo huo na Wajerumani hao.
Wakati wa utawala wa Kijerumani, nchi yetu iliitwa “Deutch – Ostafrika”; na baada ya vita ya kwanza ya Dunia mwaka 1918, ambapo Waingereza walichukua nchi kutoka kwa Wajerumani, iliitwa “Tanganyika Territory”, jina lililopendekezwa na Mwingereza, Sir Cosmo Parkinson, kabla ya kuitwa kwa kifupi “Tanganyika” baada ya vita ya tatu ya Dunia, mwaka 1945.
Mipaka rasmi ya iliyokuwa “Deutch –Ostafrika” (Tanganyika), iliridhiwa Machi 22, 1921, kufuatia Mkataba wa amani uliofikiwa kati ya Uingereza na Ujerumani ambapo, kabla ya hapo, eneo lote la sasa la Kigoma na Biharamulo, lilikuwa chini ya Wabelgiji.
Kwa madhumuni ya mada hiini kwamba, Mlima Kilimanjaro upo Tanzania kwa sababu mji wa Mombasa uko Kenya, ikiwa ni matokeo ya minyukano ya mataifa mawili ya Kikoloni, Ujerumani na Uingereza.  Na hilo hatuna nguvu nalo kwa kuwa historia sharti itawale.
Hapa tunapata fundisho pia; kwamba, Watawala wetu wa leo, wanaoingia Mikataba kimbumbumbu na kizembe na kina “Karl Peters” wa zama hizi,katika madini na ardhi, kama walivyofanya Chifu Mangungu wa Musovelo [Usagara]  na Chifu Mandara wa Moshi; waelewe kwamba, wanatuweka rehani kwa wawekezaji hao chini ya ukoloni mpya, sisi na hatima yetu.  Kwa sababu hii, tusishangae kuona siku mojatukivamiwa na wawekezaji hao, wakitumia majeshi ya nchi mama, pale tutakapoamka kutoka usingizini kudai ardhi rasilimali tunazoporwa.  Huku ni kukaribisha historia kujirudia, kwa kilio na kusaga me

Jumatatu, 28 Desemba 2015

Unaijua Vyema Historia ya Mzee Mandela??: Hebu pita hapa upate japo kwa ufupi



Rais wa kwanza wa Afrika Kusini,Mzee Nelson Mandela

Imeandikwa na Abubakari jumbe wa   Africatradition.blogspot.com.                  


Kila ifikapo18 Julai ni kumbukumbu ya kuzaliwa Mzee Nelson Mandela, rais wa kwanza wa Afrika Kusini ya Kidemokrasia (18.07.1918). Kadri ya kumbukumbu zangu huyu ndiye mtu pekee ambaye Umoja wa Mataifa umemtengea siku katika mwaka mahususi kwa heshima yake. Hivi leo anatimiza miaka 93 toka azaliwe; ni mmoja kati ya viongozi wachache wa Afrika ambao wameishi kwa muda mrefu.

Nelson Mandela ni mtu anayepewa heshima kubwa duniani kote kwa wanaomfahamu na hata wasiomfahamu. Watu wengi hasa nje ya Afrika hususani katika jamii zinazopenda kusoma vitabu wanamfahamu kupitia kitabu chake cha "Long Walk to Freedom". Hiki ni kitabu kinachoelezea historia ya maisha yake kwa kina kabisa. Sehemu kubwa ya kitabu hicho ameandika yeye mwenyewe na tena akiwa gerezani. 

 Hili ni moja ya mambo ya kujifunza toka kwa mzee huyu-maktaba kubwa duniani kote. Tujipange tuandike historia zetu sahihi ili kuiachia jamii na dunia kwa ujumla utajiri wa mawazo kama alivyofanya mzee Mandela. Wengine tulimfahamu mzee Madiba toka enzi za utoto; tukiwa shule ya msingi tuliimba nyimbo za kutaka Mandela aachiwe huru na serikali ya makaburu. Utawala wa makabulu ulitawala Afrika Kusini kwa mabavu na kwa misingi ya kibaguzi ya rangi za binadamu; ni udhalimu wa aina yake kwa ustawi wa wanadamu.

Kwanini mzee huyu ni maarufu?

Kwa hakika sifahamu yote juu ya mzee huyu anayependwa mno si tu kwake huko Afrika Kusini bali pia duniani kote kwa ujumla, hilo ladhihirika kwa Umoja wa Mataifa (UM) kumtengea siku maalum ya kumuenzi.
Mandela, alifungwa katika magereza tofauti kwa jumla ya miaka 27; umri wa kijana aliyekomaa. Mwanasiasa huyo, ambaye alikuwa pia Mwanasheria, mwanamichezo na mpigania haki za watu, alifungwa na serikali ya Makaburu kwa walichokiita uhaini. 

Nelson Mandela moja ya vijana walionzisha madai ya uhuru kwa njia ya mapigano alikuwa na imani kuu juu ya haki sawa kwa watu wote. Aliamini na anaamini kuwa binadamu wote ni sawa katika misingi ya ubinadamu- kwa haki na mahitaji yetu. Ni kwa imani na msukumo huo wa kudai uhuru na haki za watu wote wa Afrika Kusini ndo alikuwa tayari kudai haki hizo hata kama ingemlazimu kuyatoa maisha yake; funzo kubwa hilo.

Kwa hakika imani juu ya haki sawa kwa watu wote ni funzo na changamoto kubwa kwa viongozi wote duniani. Nini imani yako wewe kiongozi juu ya haki sawa kwa wananchi unaowaongoza? Ni dhahiri kuwa unatambua kuwa wananchi wako wote wanahitaji chakula cha kutosha, makazi, huduma muhimu za kijamii; afya, elimu, na kadhalika (nk). 

Lakini tunacho kishuhudia hii leo ni ubinafsi mkubwa wa viongo na hata wananchi wengine wenye nafasi bila kujali mahitaji ya wengine wenye haja ya vile vitu tu vya msingi. Wasomi wengi katika nchi zetu zinazoendelea tunahangaika na mahitaji ya ziada ila hali kuna wenzetu wengi tu wasio na mahitaji yao ya lazima. Tukitaka kutambulika vyema hapa duniani ni lazima tujifunze kwa mzee Mandela kujisahamu kwa ajili ya wengine.

Baada ya kuachiwa huru mwaka 1990 alirejea kwenye harakati za kudai haki za Waafrika Kusini walio wengi. Mwaka 1991 alichaguliwa rais wa "African National Congress" ANC Mandela alichaguliwa kuwa rais wa kwanza wa Afrika Kusini ya kidemokrasia mwaka 1994. Alitumikia muhula mmoja tu wa miaka mitano na mwaka 1999 kuacha mamlaka ya dola kuu kabisa kiuchumi barani Afrika. Utaona kuwa Mzee Madiba alifanya kinyume kabisa na viongozi wengi wa barani mwetu.

Suala kuu ambalo dunia imejifunza toka kwa mzee huyu wa miaka 93 sasa ni moyo wa msamaha. Kumbe hata kwa binadamu msamaha unawezekana. Msamaha huu umeongozwa na busara kuu bila shaka na neema tele za Mwenyezi Mungu. 

 Rais Nelson Mandela angeweza kabisa kulipa kisasi cha Waafrika Kusini weusi wengi waliopoteza maisha kwenye harakati za kujikomboa, lakini hakufanya hivyo, alisamehe na badala yake aliwaunganisha wananchi wote wa Afrika Kusini mpya, ingawa kuna vidonda vingi na makovu watakayoishi nayo daima, na kuanza kuijenga nchi yao kwa manufaa yao wote. 

Hii ni changamoto kuu kwa wanadamu wote - nadhani ni sababu hii hasa ndo imeulazimu Umoja wa Mataifa kuanzisha siku mahususi kumuenzi mpigania haki za binadamu Nelson Mandela Madiba. Kwa hakika Madiba ni mjenga dunia!!

Ukoloni ni Nini??

Ramani ya ukoloni duniani mwishoni mwa Vita Kuu ya Pili ya Dunia mwaka 1945.
Ukoloni ni mfumo wa taifa moja kuvuka mipaka yake na kutawala maeneo ya mbali yanayokaliwa na watu wengine kwa nyanja za kiuchumikiutamadunina kijamii. Maeneo haya yanaweza kuitwa koloni au eneo lindwa.
Ukoloni unaitwa hasa kipindi tangu karne ya 15 ambako Ureno na Hispaniazilianza kuenea Afrika na Amerika ya Kusini na kudumu hadi baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Lakini kulikuwa na vipindi vya ukoloni pia zamani katika historia kama vile ukoloni wa Roma ya Kale, ukoloni wa Waarabu na vingine. Ukoloni kwa maana hii inaweza kuwa tofauti na kuundwa kwa koloni katika vipindi mbalimbali vya historia ambako maeneo bila wakazi au penye wakazi wachache sana yaliingiliwa na watu kutoka sehemu nyingine.

Nchi za Afrika ziliwekwa chini ya ukoloni wa nchi za Ulaya mara baada yaMkutano wa Berlin ulioitishwa nachansella wa Ujerumani Bismarckmwaka 1884-1885.
Nchi zilizojenga ukoloni huu wa Afrika zilikuwa UingerezaUfaransaUreno,UjerumaniUhispaniaItalia na Ubelgiji.
Ukoloni mamboleo ni aina ya nchi au kundi la nchi fulani kutawala nchi nyingine kinyemela kwa kuweka vikwazo na masharti yatakayowafanya watawaliwa waendelee kuwa na uchumi tegemezi ili wawatajirishe zaidi hao wanaowatawala kinyemela